27 Julai 2026 - 13:17
Bernie Sanders: Vita dhidi ya Iran inakiuka Katiba ya Marekani

Seneta Bernie Sanders amesema kuwa vita dhidi ya Iran ni kinyume cha Katiba ya Marekani na hakikupaswa kamwe kuanzishwa, akitoa wito wa mazungumzo na kusitishwa kwa vita hiyo haraka iwezekanavyo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Bernie Sanders, Seneta huru wa Jimbo la Vermont nchini Marekani, amekosoa vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akisema kuwa vita hivyo ni kinyume cha sheria na vinakiuka Katiba ya Marekani.

Sanders amesema kuwa vita hivyo visivyo halali dhidi ya Iran havikupaswa kamwe kuanzishwa, akisisitiza kwamba Marekani inapaswa kutafuta njia za kidiplomasia badala ya kuendeleza mzozo wa kijeshi.

“Tunapaswa kukaa chini, kufanya mazungumzo na kumaliza vita hivi haraka iwezekanavyo,” alisema Sanders, akitoa wito wa kutafuta suluhisho kupitia mazungumzo.

Seneta huyo wa Marekani pia amekosoa sera ya Washington ya kuendelea kujihusisha katika migogoro ya kijeshi katika Mashariki ya Kati, akisema kuwa Marekani haipaswi kuendelea kuhusika katika kile alichokiita “vita vya mauaji ya kimbari vya Israel huko Gaza,” wala kushiriki katika uharibifu wa Lebanon.

Kauli ya Sanders imekuja wakati mjadala kuhusu uhalali wa kisheria na kisiasa wa hatua za kijeshi za Marekani dhidi ya Iran ukiendelea nchini humo, huku baadhi ya wanasiasa wakitaka Washington itumie njia za kidiplomasia na kuacha sera za kuingilia migogoro ya kijeshi katika eneo la Mashariki ya Kati.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha